Wednesday, November 23, 2016

Kuna hali mzozo ndani ya magereza ya Uholanzi kutokana na uhaba wa wafungwa..

Huku maeneo mengi ya dunia yakihangaika na magereza yaliyojaa wafungwa kupita kiasi, Uholanzi ina tatizo tofauti . Uchache wa wafungwa . Katika kipindi cha chini ya miaka 19, magereza yamefunga shughuli zake na mengine zaidi yamepangwa kufungwa mwaka ujao. Ni vipi hili liliwezekana - na kwa nini baadhi ya watu wanafikiri ni shida?
Harufu nzuri ya kupendeza ya vitunguu inanukia, kupitia mlilango ya mahabusu na katika jengo zima . Jikoni wafungwa wanaandaa chakula chao cha jioni . Mwnamume mmoja aliyeko upande mmoja wa jiko anakata mboga.
"Nilikuwa na miaka sita ya kujifunza sasa nina uelewa zaidi wa shughuli hii!" alisema.
Ni kazi yenye kelele kwa sababu kisu kimefungwa kwenye nyororo ndefu iliofungwa juu.
"Hawawezi kuchukua kisu hicho mikononi ," anasema Jan Roelof van der Spoel, naibu gavana wa gereza la Norgerhaven, lenye ulinzi mkali lililoko kaskazini mashariki mwa Uholanzi. "Lakini wanaweza kuazima visu vidogo vya jikonikama wakitoa vitambulisho vyao ili tufahamu ni nani ana nini"
Baadhi ya wanaume hao wamefungwa kwa kufanya makosa ya ghasia na wazo kwamba watembee na visu ni suala linalotia shaka. Lakini kujifunza kupika ni moja tu ya njia ambazo gereza husaidia wafungwa kurejea katika maisha ya kawaida mara baada ya kufunguliwa.Katikka magereza ya Uholanzi tuanaangalia kila mmoja ," anasema Van der Spoel.
" Kama mtu fulani ana matatizo ya mihadarati tunatibu hali yake, kama ni wenye hasira tunawapatia ushauri wa kudhibiti hasira zao , kama wana matatizo ya pesa tunawapatia ushauri nasaha. Kwa hiyo tunajaribu kuondoa kile kinachosababisha mtu afanye uhalifu . Mfungwa mwenyewe lazima awe na utashi wa kubadilika lakini njia yetu imewafaa sana. Kwa zaidi ya miaka 10 , kazi yetu imeboreka zaidi na zaidi.''
Wafungwa wanaofuata maelekezo hatimaye hupewa kifungo cha miaka miwili na msururu wa mafunzo katika mpango wa kuwarejesha katika hali ya kawaidi . Chini ya 10% hurejea gerezani baada ya kuachiliwa huru.
Hewa safi ni muhimu kwa hiyo wafungwa huruhusiwa kutembea wakisindikizwa hadi maktaba , kwenye kliniki ama mgahawa na hilo huwasaidia kuendelea na maisha ya kawaida punde wanapomaliza kifungo cha gerezani.chanzo na bbc swahili

No comments:

Post a Comment